VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Sunday, April 24, 2016

Tishio la usalama linalokabili eneo la mpaka wa Kenya na Somalia sasa Bomba la mafuta la Uganda litapitia Tanzania

Kator fm (File)
Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametangaza kuwa bomba la mafuta la Uganda kutoka Hoima hadi Bandari ya Tanga litapitia Tanzania, mradi ambao unatarajiwa kugharimu dola za kimarekani bilioni 4.
Viongozi hao wamefanya uamuzi huo kwenye Mkutano Mkuu wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika mjini Kampala, ambao pia umeamua kuwa bomba jingine la mafuta litajengwa nchini Kenya kutoka eneo la Lokichar hadi bandari ya Lamu.
Vyombo vya habari vya Uganda vimeona kuwa, uamuzi wa kujenga bomba hilo kupitia Tanzania unatokana na tishio la usalama linalokabili eneo la mpaka wa Kenya na Somalia.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/25/1s152805.htm 

Nguli wa muziki wa Rhumba, Papa Wemba afariki dunia

Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba, anaejulikana kwa jina maarufu Papa Wemba, ameiaga dunia akiwa katika jukwaa Jumapili Aprili 24. Mwanamuziki huyu nguli wa Congo (DRC) alikuwa na udhaifu wakati wa tamasha aliloendesha nchini Cote d'Ivoire Jumamosi Aprili 23.http://www.kiswahili.rfi.fr/utamaduni/20160424-gwiji-wa-muziki-wa-kiafrika-papa-wemba-afariki
Papa Wemba, mwimbaji na mtunzi wa Muziki wa Afrika.
© E. Sadaka
 Msemaji wa serikali, Lambert Mende imeelezea huzuni ilio nao kwa kumpoteza msanii


mkuu Papa Wemba, mfalme wa muziki wa Rumba.
Nyota wa soka wa Cameroon, Samuel Eto'o, ameelezea kuwa ana huzuni mkubwa kuona amemkosa gwiji wa muziki wa Kiafrika.
Waandaaji wa tamasha la miziki ya miji ya Anoumabo (FEMUA), ndio wametangaza kifo chake Jumapili asubuhi. Papa Wemba alikuwa na umri wa miaka 66. Raia wa Afrika ya Kati na kungineko wamejawa na huzuni na hisia.


Papa Wemba alikua na udhaifu wakati wa tamasha alilopiga mjini Abidjan, Jumamosi, Aprili 23, katika tamasha la FEMUA 2016, ikiwa ni tamasha la miziki ya miji ya Anoumabo. Amefariki alipofikishwa hospitalini Jumapili asubuhi, baada ya kuanguka ghafla akiwa jukwaani. Kifo chake kimetangazwa saa sita mchana na waandaaji wa FEMUA.
Udhaifu kwenye jukwaa
Hisia kubwa na huzuni mjini Abidjan Jumapili hii, mwandishi wetu, Olivier Rogez, amearifu. Mwanamuziki, ambaye alikua akihitimisha tamasha hilo, alikuwa kwenye jukwaa saa 11:00 alfajiri. Kulikua na joto kubwa na Papa Wemba alikua na ishara ya uchovu. Aliomba mara kadhaa kuongeza sauti ya vipaza sauti. Mwanamuziki huyo nguli wa Congo alianguka alipokua akiimba mwimbo wa nne.
Papa Wemba aliondolewa kwenye jukwaa baada ya kupoteza fahamu. aliondolewa sehemu hiyo na timu za waokoaji, Olivier Rogez amearifu, na kusafirishwa katika hospital ya karibu lakini mwanamuziki huyo hakuwa na muda tena wa kuishi duniani. "Wakati nitakua bado na uwezo wa kuimba, nitaimba," alisema Papa Wemba siku chache kabla ya kifo hicho kumkuta, ametoa ushuhuda Claudy Siar akiwa mjini Abidjan, ambako pia anahudhuria tamasha la FEMUA kwa niaba ya RFI.
Mwanamuziki nguli wa muziki wa Rumba
Papa Wemba alizaliwa mwezi Juni 1949 katika jimbo la Kasai-Masharikil (DRC), na alikua gwiji wa muziki wa Kiafrika. Katika miaka ya 1950, muziki wa Rumba kutoka Congo ulitawala barani Afrika na bado unatikisa na kuchezwa jukwaa mbalimbali barani la Afrika. Papa Wemba pamoja na bendi ya Zaiko Langa Langa waliinua Rumba kwa kiasi fulani na kweza kuchezwa katika jukwa za kimataifa.
Wasifu wa Papa Wemba
Papa Wemba alikuwa mwanzilishi wa studio na bendi ya Viva la Musica mwaka 1977, na alicheza nyimbo kama vile Analengo mwaka 1980, na baadaye Maria Valencia au Yolele, nguli wa "muziki wa dunia". Ni kwa msaada wa mwanamuziki wa Uingereza Peter Gabriel ndiye alimfanya Papa Wemba kujulikana duniani.
Papa Wemba aligundua na aliweza kuvipa mafunzo vizazi vya wanamuziki wa Afrika kama Koffi Olomide.
Papa Wemba alishiriki katika vipindi vingi vinavyorushwa hewani na RFI.
http://www.kiswahili.rfi.fr/utamaduni/20160424-gwiji-wa-muziki-wa-kiafrika-papa-wemba-afariki

 

Friday, April 22, 2016

Uganda mwenyeji wa mkutano kuhusu miundombinu


ICGLR, Kampala, Agosti 7, 2012.
REUTERS/Edward Echwalu

    
 
Marais wa Kenya, Uganda, Rwanda na Sudan Kusini wanatarajiwa kukutana kesho jijini Kampala nchini Uganda katika kikao cha 13 kujadili kuhusu maendeleo ya miundo mbinu zinazounganisha nchi hizo nne.







Miongoni mwa miradi ambayo mataifa hayo yanashirikiana ni pamojana ujenzi wa reli ya Kati na ujenzi wa bomba la kusafiria mafuta.
Inaelezwa kuwa, Uganda inatarajiwa kufafanulia Kenya kwenye kikao hicho ni kwanini umeamua kujenga bomba lake la kusafirishia kupitia bandari ya Tanga.
Hayo yakijiri, viongozi wa Kenya, Uganda na Tanzania mwishoni mwa wiki wanatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda na Kenya hadi pwani.
Mwaka jana, Kenya na Uganda zilikuwa zinashauriana kuhusu mpango wa kujenga bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima, magharibi mwa Uganda, hadi bandari ya Lamu katika Pwani ya Kenya.
Bomba hilo la mafuta lilikusudiwa kutumiwa kusafirisha mafuta ghafi kutoka eneo la Ziwa Albert nchini Uganda na kutoka eneo lenye mafuta la Lokichar nchini Kenya.
http://www.kiswahili.rfi.fr/eac/20160422-uganda-mwenyeji-wa-mkutano-kuhusu-miundombinu


Serikali ya Tanzania ndio mmiliki wa kampuni ya General Tyres Arusha


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, wa Tanzania Bw Charles Mwijage amesema hivi sasa kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre Arusha kinamilikiwa na serikali baada ya serikali kununua asimilia 26 kutoka kwa mbia wake. Akizungumza bungeni, Bw Mwijage amesema serikali imeweka dhamana ya kusimamia na kuendesha kiwanda hicho, chini ya shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kwamba tangazo la Serikali (GN) kuhusu uamuzi huo litatolewa wakati wowote kuanzia sasa. Amesema dhamira ya serikali ni kuona kiwanda hicho kinaanza kuzalisha matairi mapema iwezekanavyo. Pia shirika hilo litatoa majibu ya kiufundi na kijamii na kwamba ni lazima lizingatie maoni ya wadau wa sekta husika kwa ajili ya kuboresha kiwanda hicho. Aidha, mradi huo utaendeshwa chini ya menejimenti ya rasilimali watu wenye weledi katika biashara ya matairi na bila kutegemea ruzuku kutoka serikalini. Awali kiwanda hicho kiliacha uzalishaji mwaka 2009 baada ya serikali kukosa fedha za kukiendesha huku mbia mwenza kampuni ya Continental AG, kutokuwa tayari kuendelea na uwekezaji huo.
 http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152770.htm

Ukuaji wa sekta ya viwanda bado uko nyuma Tanzania


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya bajeti nchini Tanzania imesema ukuaji wa sekta ya viwanda katika awamu ya kwanza ya mpango wa maendeleo ya taifa ulikuwa chini ya lengo, jambo ambalo haliridhishi maendeleo ya uchumi wa viwanda.
Akizungumza na radio China kimataifa, mwenyekiti wa kamati hiyo Hawa Ghasia amesema ukuaji wa sekta ya viwanda katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango huo ulikuwa asilimia 6.6 chini ya lengo la kufikia wastani wa asilimia 11 mwaka 2015.
Amesema jambo hilo haliridhishi maendeleo ya uchumi wa viwanda na kusisitiza kuwa sekta ya madini katika utekelezaji wa mpango wa awamu ya kwanza haukuwa na mabadiliko makubwa kwenye Pato la Taifa kwa mwaka 2010. Kwa upande wake, naibu msemaji wa upinzani bungeni wa wizara ya fedha na Mipango Bw David Silinde amelitaka bunge kupitisha azimio ili kamati ya bunge kuhusu bajeti iwasilishe muswada wa sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo.

http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152771.htm 

Tanzania kuanza kutekeleza ahadi ya Magufuli

Serikali ya Tanzania imesema itaanza kutekeleza ahadi ya rais John Magufuli ya kukipa kila kijiji nchini Shilingi milioni 50 katika mwaka wa fedha wa 2016-2017.
file katoro fm
Akizungumza bungeni, naibu waziri ofisi ya rais, Bw Antony Mavunde amesema utaratibu wa kugawa fedha hizo unaandaliwa na baraza la uwezeshaji wananchi kwa kushirikiana na wizara ya Utawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.Ameongeza kuwa vigezo ambavyo vimekuwa vikitumika katika kutoa mikopo na mitaji kwa vijana ni umri usiozidi miaka 35 ambapo vijana watahitajika kujiunga na Saccos za wilaya na kuunda vikundi na kuvisajili kisheria.Amesema ili kuhakikisha vijana wanakuwa wajasiriamali na wanaweza kupatiwa mikopo na mitaji, serikali imejiwekea mikakati ya kutambua vijana na mahitji yao katika ngazi mbalimbali na kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa makundi mbalimbali ya vijana.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152772.htm 

Wednesday, April 20, 2016

Wafanyabiashara 13 kutoka nchini Oman wawasili mkoani Mtwara nchini Tanzania kuangalia fursa za uwekezaji

Picha File Katoro Fm
Wafanyabiashara 13 kutoka nchini Oman wamewasili mkoani Mtwara nchini Tanzania kuangalia fursa za uwekezaji na jinsi watakavyoshirikiana na Watanzania katika masuala ya kiuchumi.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego alisema mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kuwasili kwa wawekezaji hao ni fursa ya pekee kwa mkoa huo.
Alisema wafanyabiashara hao wamelenga kuwekeza katika maeneo mbalimbali ikiwamo sekta za kilimo, utalii, gesi na mafuta.
Kaimu Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asili Madimba, Mhandisi Nkilila Lucas alisema wafanyabiashara hao wana jukumu la kuwekeza katika sekta ya mafuta na gesi.
Mfanyabiashara kutoka Oman, Mansul Hemed alisema ziara hiyo imelenga kuangalia shughuli za uwekezaji na jinsi watakavyoweza kutoa elimu.
Alisema wafanyabiashara wa Kitanzania kwa sasa wanaweza kupeleka bidhaa zao Oman kama vile mifugo na mazao yanayolimwa nchini.
Wafanyabiashara hao wamewasili nchini na kutembelea maeneo mbalimbali yenye fursa za kiuchumi
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/20/1s152718.htm 

Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania atoa onyo la ugonjwa wa mnyauko katika mikorosho kwa wakulima

Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Mfaume Juma(file Katoro fm)
Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Mfaume Juma amesema kuingia kwa ugonjwa wa mnyauko katika mikorosho ni tishio katika zao hilo na kuwapa hofu wakulima.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mtwara mwishoni mwa wiki iliyopita, Juma alisema ugonjwa huo unaweza kukausha mikorosho kwa muda mfupi.
Aliwataka wakulima kutoa taarifa za kuingia kwa ugonjwa huo kwenye maeneo yao ili waweze kupatiwa elimu jinsi ya kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo.
Juma alisema licha ya kuwapo kwa wataalamu wa kutosha nchini wa kuweza kuyabaini magonjwa na kuyafanyia utafiti, bodi hiyo imefanya jitihada mbalimbali kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti Naliendele ili kuona watakavyosaidia wadau wa zao hilo kupambana na kuondoa ugonjwa huo.
Mtafiti kiongozi wa korosho ambaye pia ni mtaalamu elekezi wa zao hilo barani Afrika wa kituo hicho, Profesa Peter Masawe alisema ugonjwa huo umekuwa ukiathiri mikorosho ya zamani na unasambaa kwa kasi zaidi
Zao la korosho
.
Profesa Masawe alisema baada ya kuibuka kwa ugonjwa huo nchini kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walifanya utafiti na kubaini kuwa ni fangasi.
Aliiomba Serikali kuwekeza fedha katika tafiti kutokana na kutumia fedha nyingi.
Mtafiti mstaafu wa kituo hicho, Dk Shomari Shamte alisema ugonjwa huo unasababishwa na vimelea aina ya uyoga ambavyo vinajulikana kama Fusarium oxysporum.
Alisema hali hiyo husababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa yanayochangia vimelea hivyo kushambulia mikorosho kutokana na kuwa na uwezo wa kuishi.
 http://swahili.cri.cn/141/2016/04/20/1s152719.htm

Tuesday, April 19, 2016

Mfugaji wa Tanzania ashinda tuzo ya kimataifa ya mazingira

Bw Edward Loure.mshindi wa tuzo ya mazingira ya Goldman kwa mwaka huu
Mfugaji wa kabila la wamaasai kutoka Tanzania ameshinda tuzo ya mazingira ya Goldman kwa mwaka huu, kutokana na njia yake ya kipekee ya kulinda mazingira na jamii yake kwa ujumla.
Tuzo hii inatolewa kila mwaka katika mabara yote kwa watu hodari kwenye uhifadhi wa mazingira, ili kuwatambua wanaharakati jasiri kwa mchango wao katika kuhifadhi mazingira na jamii zao. Mwaka huu tuzo hiyo kwa bara la Afrika imeenda kwa Bw Edward Loure.
Bw Loure ameshinda tuzo hiyo kutokana na juhudi zake katika kuhakikisha ekari laki mbili za ardhi katika eneo la jamii yake zinapatiwa haki miliki ya jamii yake, na si watu binafsi.
Tuzo ya mazingira ya Goldman ilianzishwa mwaka 1989 na viongozi wa kiraia wa San Fransisco, na washindi wanachaguliwa na jopo la majaji wa kimataifa kutokana na majina yanayopendekezwa na mtandao wa kimataifa na watu binafsi.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/19/1s152662.htm 

Daresalaam Tanzania:Wananchi kuwezehswa kiuchumi

Katoro FM (File)
Baraza la Taifa la Tanzania la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC) limewataka waratibu wa uwezeshaji katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, kutumia mafunzo waliyopata kulisaidia baraza hilo kufikia malengo yake ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Beng'i Issa amesema waratibu hao wana wajibu wa kuhakikisha wanatumia ujuzi walioupata kwa faida ya wananchi katika mikoa yao.
Jumla ya waratibu 41 wa madawati ya uwezeshaji kutoka katika mikoa ya Ruvuma, Iringa, Njombe, Rukwa, Songwe na Mbeya walipatiwa mafunzo ya siku tatu jijini Mbeya.
Mafunzo hayo yalimalizika mwishoni mwa wiki na waliopewa mafunzo wametakiwa kufanya kazi kwa niaba ya baraza kutekeleza sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Alisema mafunzo hayo yamelenga kuwapatia ufahamu wa kujua wajibu wao, kufanya kazi na jamii, kuibua fursa, kuwaonyesha fursa wananchi na kuwaunganisha na vyombo vya fedha na mifuko ya serikali kupata mikopo kuendeleza shughuli za kijasiriamali.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa NEEC, mafanikio na changamoto zitakazojitokeza katika kanda hiyo zitatumika katika kuboresha kanda nyingine zilizobaki.

http://swahili.cri.cn/141/2016/04/19/1s152677.htm

Mugabe alalamikia askofu kuhusu ndoa za jinsia moja

Rais Mugabe hupinga sana wapenzi wa jinsia moja
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe alikutana na Askofu mkuu wa Canterbury na kuibua maswali kuhusu ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Askofu mkuu Justin Welby amesema alimjibu kiongozi huyo kwamba kuna mitazamo tofauti kuhusu ndoa hizo miongoni mwa waumini wa kanisa la Kianglikana kote duniani.
Aliongeza hata hivyo kwamba wengi wa waumini wanaamini ndoa ni uhusiano wa muda mrefu baina ya mwanamume na mwanamke.
Askofu Welby alisema ni makosa kuwahukumu au kuwaadhibu watu kwa sababu ya msimamo wao kijinsia na kimapenzi.
Hata hivyo, amesema dalili zilionesha Bw Mugabe hakukubaliana naye.
“Sidhani itakuwa haki kusema kwamba Bw Mugabe alikubaliana name kabisa,” alisema Askofu Welby.
Mkutano huo wa faraghani ulifanyika mjini Harare, baada ya Askofu Welby, ambaye yumo katika taifa jirani la Zambia anakohudhuria mkutano wa viongozi wa kanisa la Kiangilikana kufanya ziara fupi Zimbabwe.
Msemaji wa Lambeth Palace amesema mpango huo ulipangwa dakika za mwishomwisho na ulidumu chini ya saa moja.
Bw Mugabe ni Mkatoliki na hupinga sana ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Askofu Welby amesema Bw Mugabe hakukubaliana naye kabisa
Maafisa wa kanisa hilo wamesema mkutano huo ulikuwa sana wa kidini badala ya kisiasa ingawa uhusiano baina ya serikali na kanisa ulijadiliwa.
Mwandishi wa BBC Callum May anasema mkutano huo ndio wa kwanza kufanyika kati ya askofu mkuu wa kanisa la Kiangilikana na Bw Mugabe tangu 2011 uhusiano kati ya kanisa hilo na serikali ulipokuwa umedorora sana.
Askofu Welby amesema hali kwa sasa imeimarika sana.
Suala la kutambuliwa kwa ndoa wapenzi wa jinsia moja limekuwa likizua mgawanyiko hasa katika kanisa la Kianglikana duniani, zikipingwa sana na majimbo ya kanisa hilo barani Afrika..
Januari mwaka huu viongozi wa kanisa hilo waliokutana Canterbury, walisisitiza kwamba ndoa ni kati ya mwanamume na mwanamke na likasimamisha ushirika wa jimbo la Marekani lililotambua ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Walisema kanisa hilo lilikiuka Imani inayofuata na waumini wengi wa kanisa la Kianglikana kuhusu ndoa.
http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160419_mugabe_same_sex_marriage 

DARAJA LA KIGAMBONI SASA NI DARAJA LA MWL. NYERERE

Rais Magufuli ametoa tamko hilo kwa Waziri wa Ujenzi, kulipa jina la Nyerere ikiwa ni kuenzi kazi kubwa aliyoifanya baba wa taifa ya  kuwaunginisha watanzania.
Hayo ameyasema muda si mrefu katika uzinduzi wa daraja hilo maarufu kama Daraja la Kigamboni. Daraja ambalo ni la pekee Afrika mashariki na kati, amablo limegharimu yapata bilioni 254Tsh.

Rais Magufuli
Faida kwa watu wa hali ya chini, ambao Kwa Dk. Magufuli jicho lake linawaangalia kwa jicho la huru, hao watapita bure bila tozo, bali kwa wale wenye vyombo vya usafiri watachangia kwa kulipia usafiri huo.
Daraja limejengwa kwa ushirikiano wa Serikali kuu na NSSF ambao wachangia asilimia 60 ya mradi amabyo inapsaswa kurudishwa ili kusaidia pahala pengine penye uhitaji.

Monday, April 18, 2016

Daraja la kisasa kuzinduliwa Kigamboni

File
Rais Joseph Pombe Magufuli wa Tanzania atafungua daraja la Kigamboni hapo kesho.
Daraja hilo litaunganisha eneo la Kigamboni na mji wa Dar es Salaam.
Ujenzi wa daraja hilo umegharimu zaidi dola milioni 140.
Daraja la Kigamboni linatarajiwa kurahisisha usafiri na uchukuzi jijini humo.
Daraja hilo ndilo daraja refu zaidi Afrika Mashariki linalobeba uzito kwa nyaya.

 http://www.bbc.com/swahili/medianuai/2016/04/160418_kigamboni_bridge

Tanzania: Bajeti ya Afya imeongezwa Hadi 250bn Kutoka 41bn

.Bi Ummy Mwalimu (Katoro Fm File)
Serikali ya Tanzania imeongeza bajeti yake kwa ajili ya ununuzi wa dawa kutoka sh bilioni 41 katika mwaka wa fedha wa 2014/15 hadi sh bilioni 251 katika mwaka wa 2015/16 kushughulikia uhaba wa dawa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na Wazee, Bi Ummy Mwalimu, anasema mwishoni mwa wiki iliopita serikali ya Awamu ya Tano imejiandaa vizuri ili kuhakikisha kwamba hakuna mgonjwa atakufa kutokana na uhaba wa dawa kwa sababu katika mwaka huu wa fedha, imetenga fedha za kutosha kwa ajili ya ununuzi dawa.
Waziri huyu pia amewahakikishia wananchi ambao watapatikana na maambukizi ya virusi watapata dawa za kutosha.


http://swahili.cri.cn/141/2016/04/18/1s152640.htm 

Sunday, April 17, 2016

Watoto Geita walazimika kuchagua kati ya chakula na masomo

Ingawa serikali ya Tanzania inataka kutoa elimu kwa kila mtoto, baadhi ya watoto wa mkoani Geita wamesema wanapendelea kufanya kazi migodini au kuvua samaki kwani familia zao hazina pesa ya kutosha na hawataki kulala njaa. Hawa Bihoga amewatembelea na kushuhudia hali ya maisha yao.

fuatilia link kwa habari zaidihttp://www.dw.com/sw/watoto-geita-walazimika-kuchagua-kati-ya-chakula-na-masomo/av-19183127

Annan: Nkurunziza hakustahili kuwania urais

Rais Nkurunziza
Aliyekuwa Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa bwana Kofi Annan amemkosoa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kwa kuwania muhula wa tatu.
Bw Annan amesema Nkurunziza anafahamu vyema kuwa ni kinyume cha katiba ya taifa hilo kuwania madaraka kwa zaidi ya vipindi viwili.

Raia huyo wa Ghana anamlaumu rais Nkurunziza kwa kusababisha maandamano yaliyosababisha vifo vya takriban watu mia nne.
Bw Annan ameiambia BBC kuwa bw Nkurunziza haoneshi dalili zozote za kutafuta suluhu la amani wala nia ya kutaka mazungumzo ya kweli na wapinzani wake.
Bw Annan ameiambia BBC kuwa bw Nkurunziza haoneshi dalili zozote za kutafuta suluhu la amani.

Katibu huyo wa zamani ameiomba jamii ya imataifa kuyasaidia mataifa ya Afrika yanayokabiliwa na matatizo chungu nzima kama vile Ethiopia inayokabiliwa na baa la njaa
Annan anasema kuwa mataifa hayo ya Afrika yamesahaulika huku kurunzi ya ulimwengu ikiangazia Syria na mataifa ya Mashariki ya kati http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160417_annan_on_burundi

Filamu nyingine ya Avatar kuongezwa

Watengenezaji wa filamu ya Avatar franchise wamesema kutatolewa filamu zaidi katika mwendelezo huo wa filamu, filamu ijayo ikitarajiwa kutolewa 2018.
Mwelekezi wa filamu hizo James Cameron ametangaza kwamba filamu hizo zitaendelezwa hadi makala ya tano itakayotolewa 2023.
Alikuwa tayari amethibitisha kwamba filamu tatu zaidi zingetolewa lakini amefichua kwamba kuna mambo mengi sana ya kuelezwa kwenye hadithi hiyo na makala zijazo tatu hazitoshi.
Kote duniani, Avatar inasalia kuwa filamu iliyofanikiwa zaidi katika historia.
Filamu hiyo imezoa $2.7bn tangu kutolewa wake 2009.
Filamu ijayo ya Avatar itatoka 2018, na hizo nyingine 2020, 2022 na 2023.

http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160416_avatar_fifth

Tanzania yaweka mipango ya kupunguza msongamano wa magari

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DK.Magufuli(file)
Rais John Magufuli wa Tanzania ametangaza mipango ya kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam.
Amesema baadhi ya mipango hiyo ni pampja na kuwekeza ujenzi wa barabara na reli katika mji huo wenye wakaazi milioni tano.
Rais Magufuli aliyasema hayo wakati akizindua ujenzi wa barabara ya juu jijini humo.
Amesema barabara ya kilomita 128 yenye laini sita itajengwa kutoka Kigamboni Bridge hadi eneo la pwani la Chalinze ikiwa na madaraja matano ya juu.
Rais Magufuli pia amesema tayari serikali imetenga dola milioni 500 kwenye mwaka ujao wa fedha kufanyia ukarabati reli ya mjini ili iwe ya kisasa.

Saturday, April 16, 2016

Tanzania yaimarisha oparesheni dhidi ya bangi


Bangi(Maktaba) ktfm
Polisi nchini Tanzania wameendeleza oparesheni dhidi ya ukuzaji wa bangi pamoja na biashara yake kwenye eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo la Arusha.
Oparesheni hiyo inaendelezwa huku ripoti ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa Tanzania ndio mzalishaji mkuu wa pili wa bangi barani Afrika.
Kamanda wa polisi kwenye eneo la Arusha Charlse Mkumbo amesema oparesheni hiyo italenga biashara na ukuzaji wa bangi na miraa.
Bangi inayokuzwa Arusha hupelekwa mjini Nairobi ambako inasambazwa kwenye nchi za Uganda, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi, Ethiopia na Sudan.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/16/1s152593.htm 

Friday, April 15, 2016

Timu 4 zatinga nusu fainali

Hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imepigwa Alhamisi hii, Aprili 14 kwa michezo minne.

Wawekezaji wa madini Tanzania wataka kujadili na serikali yao jinsi ya kuboresha mazingira ya biashara hiyo


kutoka mataba katoro fm
madini hali ambayo itawatorosha wawekezaji wa kigeni. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya maofisa wa migodi ya madini nchini humo wamesema kuna changamoto kadhaa ambazo zimechangia wawekezaji katika sekta ya madini kutowekeza kwenye utafutaji wa madini jambo ambalo linaweza kuifanya sekta hiyo kuporomoka au kudumaa.
Mwenyekiti wa Chama cha Madini na Nishati Tanzania Bw Ami Mpungwe amesema kuna haja kubwa ya serikali kukutana na wawekezaji wa madini kwa sababu kuna tabia ya kushutumiana na kulaumiana kila upande jambo ambalo linaweza kutatuliwa kwa mazungumzo. Mpungwe amesema mkutano huo ulikuwa muhimu kwa faida ya wawekezaji na serikali. Ameongeza kuwa wadau kwenye sekta ya madini wana kilio kikubwa ambacho suluhisho la uwekezaji wa sekta hiyo ni serikali kukaa na wawekezaji na kusikia malalamiko yao.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/15/1s152591.htm 

Mtazamo mpya kukabili hali ya HIV kwa wanaojichoma dawa za kulevya unahitajika:UNAIDS

Mtazamo mpya kukabili hali ya HIV kwa wanaojichoma dawa za kulevya unahitajika:UNAIDS
Sindano kama hizi zinatumiwa na watu wanaojidunga dawa za kulevya.(Picha:UM/Evan Schneider)
Kabla ya kuanza kwa kikao maalumu cha baraza kuu la Umoja wa mataifa kuhusu tatizo la mihadarati duniani , shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limetoa ripoti mpya iitwayo "Usidhuru:afya, haki za binadamu na watu wanaotumia dawa za kulevya". John Kibego na taarifa kamili.
(TAARIFA YA KIBEGO)
Kwa mujibu wa UNAIDS, ripoti hiyo inaonyesha kwamba kushindwa kwa nchi nyingi kuchukua mtazamo wa afya na haki za binadamu kumesababisha kutopungua kimataifa idadi ya visa vipya vya maambukizi ya HIV miongoni mwa watu wanaojidunga dawa za kulevya kati ya mwaka 2010 na 2014.
Mkurugenzi mkuu wa UNAIDS Michel Sidibé, amesema suala la kuchukulia maisha kama kawaida, halijaifikisha dunia popote na ni lazima ijifunze kutokana na miaka 15 iliyopita na kufuata mfano wan chi ambazo zimeweza kubadili hali ya maambukizi miongoni mwa wanaotumia dawa za kulevya kwa kuchukua mtazamo wa kupunguza madhara kwa kutoa kipaumbele kwa afya na haki za binadamu.Kama anavyofafanua msemaji wa UNAIDS Monique Middelhoff
( MONIQUE MIDDELHOFF)
"Tunachokishuhudia ni kwamba mtazamo wa upunguzaji madhara tayari ni wa kimataifa, unatekelezwa Kazakhstan, Malaysia, Uchina,Ulaya , na afrika nchi kama Tanzania na Kenya, hivyo inawezekana."
Kikao maalumu cha baraza kuu kuhusu tatizo la dawa za kulevya duniani kitafanyika April 19 hadi 21 hapa New York.
http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/2016/04/mtazamo-mpya-kukabilia-hali-ya-hiv-kwa-wanaojichoma-dawa-za-kulevya-unahitajikaunaids/#.VxHuEXovaC4 

Sudan Kusini yaingia rasmi Afrika Mashariki



Rais Kiir amesema Sudan Kusini imejiunga na jumuiya sahihi

Sudan Kusini sasa ni mwanachama mpya wa jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya Rais wa nchi hiyo Salva Kiir kusaini mkataba wa kujiunga rasmi na jumuiya hiyo.
Rais Kiir ametia saini mkataba huo jijini Dar es Salaam mbele ya mwenyeji wake Rais wa Tanzania John Magufuli ambaye kwa sasa ndiye Mwenyeketi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Amesema kujiunga kwa nchi yake na jumuiya hiyo kumemfanya kujihisi kuwa kwenye jumuiya sahihi.
“Ninaposimama hapa leo hii, moyo wangu umejawa na furaha na hali ya kuridhishwa kuwa sehemu ya jumuiya hii kuu. Kwa ujasiri kabisa ninaweza kusema hatimaye Sudan Kusini imepata mahala sahihi katika jumuiya,” alisema Rais Kiir.
Viongozi wa nchi za jumuiya hiyo waliidhinisha kukubaliwa kwa Sudan Kusini kujiunga na jumuiya hiyo kwenye mkutano mkuu uliofanyika mjini Arusha mwezi uliopita.
Sudan Kusini ndiyo nchi ya sita kujiunga na jumuiya hiyo iliyoanza kwa nchi tatu Tanzania, Kenya na Uganda. Rwanda na Burundi zilijiunga na jumuiya hiyo baadaye.
Sudan Kusini sasa inatarajiwa kufungua mipaka yake kwa ajili ya biashara. Tayari kampuni na asasi nyingi za kifedha kutoka Kenya zimefungua biashara nchini Sudan Kusini.
Wengi wanatarajia hatua ya leo itafungua fursa zaidi za kibiashara kati ya Sudan Kusini na nchi wanachama wa jumuiya.
Wadadisi wengine wanaamini kuwa baadhi ya miradi ambayo Sudan Kusini ingetaka kujumuishwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni miundo msingi ikiwemo reli na mabomba ya mafuta.
http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160415_southsudan_new_eac 

Rais wa Tanzania John Magufuli ametengua uteuzi wa Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Bw Gabriel Nderumaki.

Dkt Magufuli amemteua Bi Abdallah kuwa kaimu

Bi Tuma Abdallah, ambaye amekuwa mhariri mtendaji msaidizi wa magazeti ya serikali (TSN), ameteuliwa kuwa kaimu.
Hakuna maelezo yoyote zaidi yaliyotolewa kuhusu sababu za kutenguliwa kwa uteuzi wa Bw Nderumaki.
TSN huchapisha magazeti ya Daily News, Sunday News, habari Leo, Habari Leo Jumapili na Spoti Leo.
http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160415_magufuli_tsn

Thursday, March 17, 2016

TAMISEMI YAAGIZWA KUSIMAMIA VIZURI MIKOA NA HALMSHAURI ILI KULETA MAENDELEO TARAJIWA.

Waziri Mkuu Aagiza OR TAMISEMI Kusimamia Mikoa na Halmashauri Kuleta Maendeleo tarajiwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ameitaka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-(OR-TAMISEMI) kuhakikisha inaisimamia vizuri Mikoa na Halmashauri ili serikali iweze kupata matokeo mazuri na tarajiwa.Akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI alipoitembelea ofisi ya TAMISEMI mjini Dodoma leo, Mhe. Waziri Mkuu alisema jukumu kubwa lililopo hivi sasa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni kuhakikisha kuwa zinabuni vyanzo vipya vya mapato na kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato ya serikali.
â€Å“Hatukubaliani na uzembe kwenye idara na halmashauri za wilaya kwakuwa hivi sasa serikali ya awamu ya tano inasimamia utumishi wa uadilifu hivyo kila mmoja ahakikishe anasimamia vizuri eneo lake” alisema Mhe. MajaliwaAlisema serikali ya awamu ya tano imekusudia kuwahudumia ipasavyo watanzania wenye uelewa tofauti na matakwa tofauti na kwa kuanzia serikali imeanza kuwajenga watumishi wa serikali kutambua na kukumbuka kuwa wao ni wahudumu wa wananchi hivyo inawapasa kuwahudumia vema.
â€Å“Lazima tujenge moyo wa huruma wa kuwahudumia wenzetu, anapokuja mwananchi msikilize, muhudumie na mwelekeze eneo sahihi ili aweze kupata huduma. Lazima tusimamie na kuona maeneo yote yanafanya kazi kama ilivyokusudiwa, ili kupata matokeo tarajiwa iwe ni wajibu ya kila mmoja kuhakikisha kuwa anatoa usimamizi thabiti katika eneo lake.” alisisitiza Mhe. Waziri Mkuu.
Akimkaribisha Mhe. Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. George Simbachawene alisema TAMISEMI wapo tayari kubadilika na kufanya kazi kama kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli –HAPA KAZI TU-.

http://www.pmoralg.go.tz/newseventsinfo/habari-1100-20160121-Waziri-Mkuu-Aagiza-OR-TAMISEMI-Kusimamia-Mikoa-na-Halmashauri-Kuleta-Maendeleo-tarajiwa/ 

Naibu Waziri apiga marufuku eneo la Shule kutumika kibiashara


Naibu Waziri apiga marufuku eneo la Shule kutumika kibiashara
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo, ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, kufuta mawazo ya kubadilisha matumizi Shule ya Msingi Uhuru Wasichana kama eneo la kibiashara.
Aidha amemtaka Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Isaya Mngurumi, kutoa kipaumbele kwenye malipo ya fedha za likizo na kupandishwa daraja kwa walimu wa shule hiyo, kutokana na kufanya kazi kwenye mazingira magumu.
Pia amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha kuwa Shule hiyo haikosi karatasi maalum za kuchapishia maandishi ya nukta nundu, kwa wanafunzi wasioona.
Naibu Waziri alitoa maagizo hayo Dar es Salaam, tarehe 17 februari 2016 wakati alipotembelea shule hiyo ili kufahamu changamoto mbalimbali zilizopo.
Alisema lazima maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ya kutaka Shule ya Uhuru wasichana isibadirishwe na kutumika kwa matumizi ya kibiashara yatekelezwe.
Mheshimiwa Jafo aliitaka halmashauri hiyo kuboresha miundombinu ya shule ili iendelee kutoa elimu kwa watoto kwa sababu bado serikali inahitaji uwepo wa shule za kutosha.
â€Å“Kama bado mna mawazo ya kubadirisha matumizi ya shule ya Uhuru wasichana ni bora muyafute, nataka maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, yatekelezwe” alisisitiza.
Mheshimiwa Jafo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, alionyesha kusikitishwa na mazingira magumu wanayokabiliana nayo walimu wa shule ya Uhuru mchanganyiko, ambao wanafundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Kutokana na hali hiyo, Naibu Waziri alimuagiza Mkurugenzi na Ofisa Elimu wa halmashauri hiyo, kuongeza magodoro yanayotumiwa na wanafunzi hao kufanyia mazoezi.
Aliongeza kuwa, walimu wa shule hiyo wanapaswa kupewa kipaumbele kwenye malipo ya likizo pamoja na kupandishwa madaraja kutokana na kufanyakazi kwa moyo wa kujituma.
â€Å“Mkurugenzi sitaki kusikia malalamiko kuhusu kucheleweshwa malipo ya likizo au kupandishwa madaraja kwa walimu hawa.
â€Å“Wamekuwa wakifanya kazi kwenye mazingira magumu lakini kwa moyo wa kujitolea hivyo nataka wawe wanapewa kipaumbele zaidi kwenye maslahi yao” alisema.
Naibu Waziri alisema, serikali itatilia mkazo upatikanaji wa vifaa maalum vya kufundishia ili wanafunzi wenye mahitaji maalum waweze kusoma bila vikwazo vyovyote.
Aliwataka wazazi walio na watoto wenye ulemavu, kutowaficha majumbani bali wawapeleke shuleni kupata taaluma.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Anna Mshana, alimpongeza Waziri Jafo kwa kufika kujionea changamoto zilizopo ili ziweze kufanyiwa kazi.
Alisema, wanafunzi wenye mahitaji maalum wanahitaji uwepo wa vifaa vya kutosha vya kujifunzia.
Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1921, ina wanafunzi 64 wasioona, 22 viziwi pamoja na upofu, 79 wenye mtindio wa ubongo pamoja na wanafunzi watano wenye ulemavu wa ngozi. 

Kashfa ya rushwa: FIFA yawageukia viongozi wa zamani


Gianni Infantino, Rais mpya wa FIFA. Ijumaa Februari 26, 2016 mjini Zurich.
Gianni Infantino, Rais mpya wa FIFA. Ijumaa Februari 26, 2016 mjini Zurich.
FIFA TV

Na RFI
Enzi mpya yafunguliwa katika Shirikisho la kimataifa la Soka (FIFA), ambapo rais mpya aliyechaguliwa, Gianni Infantino, ameahidi kurejesha picha na sifa nzuri kwa FIFA kwa kupambana kwa hali na mali dhidi ya rushwa. FIFA imewataka baadhi ya viongozi wa zamani wa shirikisho hilo kujieleza.

Wiki mbili baada ya uchaguzi wa Gianni Infantino, Shirikisho la Soka Duniani limeanza kubadili mkakati katika kesi inayojulikana kama "Fifagate". Baada ya kulaumiwa na mahakama ya Marekani kwa karibu mwaka mmoja kwa ufisadi mkubwa, Shirikisho la kimataifa la Soka linaonekana kuwa limeathirika kutokana na viongozi walioza kwa rushwa ambao walitumia vibaya nafasi zao kwa kujihusisha na fedha badala ya soka.
Katika taarifa iliyotolewa Jumatano hii, Machi 16, FIFA imetangaza kwamba imeomba fidia kwa watu 41, wengi wao wakiwa maafisa wa zamani wa FIFA, na ambao kwa sasa wanatuhumiwa na mahakama ya Marekani. Kwa hivyo, Shirikisho la Soka Duniani limeomba Mwendesha Mashitaka Mkuu wa jimbo la New York kushughulikia madai yake, kama taasisi iliyofanyiwa unyonge.
Afrika Kusini yashutumiwa kununuwa michuano ya Kombe la Dunia
FIFA inataka sio tu kurejeshewa fedha ziliopitishwa mlango wa nyuma na washitakiwa, lakini pia katika kurejeshewa mishahara, marupurupu na mafao mengine ambayo walilipwa wakati wa shughuli zao katika Shirikisho. FIFA inabaini kwamba fedha hizo zinakadiriwa kufikia mamia angalau ya mamilioni ya Euro, ambapo rais mpya kuzitumia katika maendeleo ya mpira wa miguu.
Watu wanaolengwa wanatoka katika bara la Amerika. Lakini pia Afrika Kusini, ambayo inashutumiwa kutoa dola milioni kumi kama rushwa ili kuhakikisha inaandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 katika ardhi yake.
tags: Shirikisho la Soka Duniani FIFA - Gianni Infantino - Afrika Kusini
 
  http://www.kiswahili.rfi.fr/afrika/20160316-kashfa-ya-rushwa-fifa-yawageukia-viongozi-wa-zamani

Vijana wandelea kutowakilishwa katika mabunge duniani : Ripoti

Nembo ya IPU.(Picha@IPU)
Ripoti mpya ya muungano wa mabunge duniani IPU inaonyesha kuendelea kwa tatizo sugu la kutowakilishwa ipasavyo kwa vijana katika mabunge, wakati huu ambapo idadi ya kundi hilo duniani ni ikubwa kuliko wakati wowote ule.
Ripoti hiyo iitwayo uwakilishi wa vijana katika mabunge ya kitaifa 2016, iliyozinduliwa leo wakati wa mkutano kuhusu wabunge vijana unaofanyika mjini Lusaka Zambia, imeabaini kwamba ni asilimia 1.9 pekee kati ya wabunge 45,000 wana umri chini ya miaka 30.
Takwimu hizo zinaonyesha kuwa hakuan ongezeko kutokana na utafiti wa IPU wa mwaka 2014 ambapo pia ripoti imeonyesha kuwa karibu theluthi ya mabunge madogo na karibuasilimai 80 ya mabaraza ya seneti hayana hata mbunge mmoja mwenye umri wa chini ya miaka 30.
Hata hivyo ripoti mpya hiyo imetaja nchi ambazo zimepiga hatua katika kuwajumisha vijana katika mabunge yao kuwa ni Sweden, Ecuador, Finland na Norway ambazo zina asilimia 10 au zaidi ya wabunge wenye umri wa chiniya miaka 30.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mjumbe wa vijana katika Umoja wa Mataifa, Ahmad Alhendawi, amesema kuna haja ya kutafuta njia za kuwashirikisha vijana zaidi, hata kutumia teknohama.
(Sauti ya Alhendawi)
"Ningependa kusisitiza umihimu wa kutambua kuwa vijana wanataka kushiriki na wana uwezo wa kushiriki, na tusiwalaumu tu bila kujua ni kwa nini hawashiriki, kwa sababu wakati mwingine kuna vizuizi vikubwa vya kimfumo."

http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/2016/03/vijana-wandelea-kutowakilishwa-katika-mabunge-duniani-ripoti/#.VurnflKbkdU 

Tuesday, March 15, 2016

Malawi yachoma pembe za ndovu haramu

Shirika la wanyama pori la Afrika linasema kuwa ndovu takriban elfu 35 waliuwawa barani humo mwaka jana.
Pembe za ndovu haramu zikichomwa.
  Malawi ilichoma pembe za ndovu takriban mia 8 jummatatu kuonyesha nguvu dhidi ya biashara haramu ya wanyama pori. Maafisa wa forodha walikamata pembe hizo mwaka 2013, pale zilipoingizwa kwa magendo nchini Malawi kutoka Tanzania.
Wafanyakazi wa mbuga ya wanyama walichoma moto takriban tani 2.6 za pembe za ndovu katika hifas=dhi ya mbuga ya Mzuzu kaskazini mwa Malawi.
Shehena ya pembe za ndovu ilikadiriwa kugharimu dola millioni 3.
Brighton Kumchedwa ni mkurugenzi wa mbuga za wanyama pori nchini Malawi.
Bw. Kunchedwa anasema kuwa, kile wanachojaribu kuonyesha ni kuwa ulanguzi wa pembe za ndovu hauna thamani kwa sababu kuna sharia ambayo inapiga marufuku biashara ya kimtaiafa ya pemb za ndovu. Kwa hiyo kile tunachosema ni kuwa, acha usafirishaji haramu wa bidhaa za wanyama pori hususan pembe za ndovu.
Pembe hizo za ndovu zilikamatwa mwaka 2013 lakini mahakama kuu ya Mzuzu iliwapatia maafisa ruhusa ya kuchoma pembe hizo mwezi huu. Tanzania awali ilizuia kuchomwa kwa pembe hizo, ikisema inahitaji baadhi ya pembe hizo kama ushahidi kwa wa kesi mahakamani nchini tanzania.
Ndugu wawili raia wa Malawi walikamatwa wakiwa na shehena ya pembe za ndovu. Walitozwa aini ya dola elfu 5 mia 5 kwa usafirishaji haramu wa pembe za ndovu.
Hii ni mara ya kwanza kwa Malawi kuchoma pembe za ndovu walokamata. Hio inakuja kufwatia harakati banarani Afrika juu ya kuendelea kuuwawa kiharamu kwa ndovu.
Idara ya wanyama pori ya Malawi inaeleza kuwa Malawi imepoteza takriban nusu ya idadi ya ndovu walokuwa nao tangu mwaka 1980, hususan kutokana na uwindaji haramu. Taifa hilo limekuwa njiapanda kwa wasafririshaji haramu wa pembe.
Kumchedwa anasema serikali inashughulikia suala hilo sasa.
Kumchedwa anasema, pembe hizi zinatokea Tanzania kwa sababau sharia zetu ni dhaifu sana. Lakini hivi tunavyozungumza, tunatathmini sharia, ili ziwe na adhabu kali.
Biashara ya kimataifa ya pembe za ndovu ilisitishwa mwaka 1989, lakini wataalam wanasema uwindaji haramu wa ndovu umeongezeka ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya pembe za ndovu huko Asia.
Shirika la wanyama pori la Afrika, linasema kuwa ndovu takriban elfu 35 waliuwawa barani Afrika mwaka jana.
http://www.voaswahili.com/content/malawi-ivory/3236898.html

CUF yasema baadhi ya wakazi wa Zanzibar wakimbilia Mombasa

Siku kadhaa kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa marudio huko Zanzibar, Chama cha Wananchi -CUF kimesema baadhi ya wanachama wake huko kisiwani Pemba wameanza kukimbilia maporini wakitafuta uwezekano wa kutoroka kisiwani humo na kukimbilia katika mji wa Mombasa nchini Kenya ili kutafuta hifadhi ya ukimbizi.

Ripoti ya Munir Zakaria wa Zanzibar skikliza katika link hapo chini.
Hatua hii inafuatia madai ya kuwepo kwa taharuki na kamata kamata inayoendelea huko dhidi ya watu wanaodaiwa kuhusika na matukio ya kuchomwa moto kwa baadhi ya nyumba.
Uchaguzi mkuu wa marudio unatokana na kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana ambao ulisemekana uligubikwa na kasoro.
Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar bwana Mohamed Aboud alisema serikali imejipanga vizuri kuhakikisha uchaguzi wa marudio unafanyika katika mazingira ya Amani na utulivu.
Aidha aliwataka wananchi kuondokana na khofu hasa katika kipindi hiki ambacho askari katika jeshi la wananchi wa Tanzania- JWTZ wanaendelea na mazoezi yao ya kawaida ya kila mwaka huko Zanzibar.

Tanzania yaahirisha uzinduzi wa kituo cha mpakani na Kenya

Rais John Magufuli alippofungua Bunge la 11 la Tanzania.
Kuanzishwa kwa kituo kipya cha mpakani kati ya Kenya na Tanzania huko Lungalunga huenda ikachukua muda kabla marais wa mataifa hayo mawili kuzindua rasmi kituo hicho baada ya Tanzania kuomba muda kukamilisha ujenzi wa kituo hicho kwa upande wao.
Mipangilio ya kituo kimoja cha mpakani kati ya Kenya na Tanzania huko Lungalunga huenda kikachelewa kuanzishwa baada ya Tanzania kuomba muda zaidi kukamilisha upande wao.
Akizungumza na sauti ya Amerika  afisa wa forodha anayesimamia kituo hicho upande wa Kenya Pius Sokoko Kwach amesema kuwa  walipaswa kuanza shughuli za kituo kimoja mwezi huu wa tatu lakini Tanzania inachelewesha mpango huo.
Pius anasema “walituambia wanaweka mitandao yao sisi huku tuko tayari  shuhuli katika kituo cha Kenya cha uhamiaji na forodha zinaendelea , hata upande wetu kitu chao kiko tayari ni wao wamalize kisha watuambie  mara tu wakimaliza waje waianzishe kwani tayari tuko na tarakilishi tumishi zao ni wao waweke yetu upande wa Tanzania”.
Bw. Sokoko Kwach amekariri kuwa   kituo hicho  kitapunguza kucheleweshwa kwa  shughuli za biashara na wasafiri wanaotumia mpaka huo kuenda na kutoka nchini Tanzania.
Pius anaendelea kusema “ maana na umuhimu ni kupunguza  vituo vingi ambavyo vinasababisha  ucheleweshaji  shughuli  hizi za one stop border ni kupunguza ucheleweshaji unaosababishwa na  shughuli za kulipisha ushuru wa bidhaa na kuangalia wasafiri kati ya mpaka wa kenya na Tanzania.
Kampuni za mabasi zinazotumia mpaka wa Kenya na Tanzani kupitia Lungalunga zimekaribisha mipango  hiyo ya kituo kimoja mpakani.
Yusuf Kassim ni msimamizi wa kampuni ya mabasi ya Tahmeed  ya Mombasa - Daressalaam.
Aidha Yusuf ameitaka jumuiya ya Afrika Mashariki pia kufuatilia mbali swala la kadi ya ugonjwa wa manjano ambao unaendeleza rushwa hasa kwa wale ambao hawana kadi hizo wanapoingia ama kutoka Tanzania.
Bashiri Seif Saidi aliye dereva wa malori ya kusafirisha chakula cha msaada cha wakimbizi kutoka Mombasa hadi kituo cha wakimbizi cha Nyarugusu nchini Tanzania anasema bado wanalazimika kusubiri mpakani hata zaidi ya siku mbili kabla kuendelea na safari isipokuwa mpaka wa Rwanda na Tanzania.
Kituo sawia na hicho kinachounganisha kenya na Tanzania eneo la Taveta na Holili kilizinduliwa rasmi tarehe 27 mwezi Februari mwaka 2016 kama njia ya kuleta umoja katika jumuiya ya Afrika Mashariki.

http://www.voaswahili.com/content/article/3235108.html 

Rais Magufuli asema hasara ya mishahara hewa inafikia billioni 2.5 kwa mwezi

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli akitoa hotuba ya kitaifa
Rais wa Tanzania  John Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni nchini humo huku akizungumzia upotevu mkubwa wa mapato ya serikali unaotokana na kuwepo watumishi hewa
Akizungumza mara baada ya kuwaapisha wakuu hao  wa mikoa rais Magufuli amesema tatizo la wafanyakazi hewa limekuwa likigharimu serikali fedha nyingi, ambapo ametolea mfano wa uchunguzi uliofanywa katika mikoa miwili ya Dodoma na singida na kubaini takriban wafanyakazi hewa 202 katika halmashauri 14.
Amesema kutokana na hali hiyo na ikichukuliwa taswira ya nchi nzima, hasara inayokisiwa inayotokana na malipo ya mishahara hewa ya wafanyakazi nchini  Tanzania inafikia shilingi billioni 2.5 kila mwezi  huku serikali ikitumia shilingi bilioni 549 kwa mwezi kwa ajili kulipa watumishi wake hivyo amewataka kuzisimamia vyema halmashauri zao.
Wakuu wa mikoa wote 25 walioapishwa baadaye wamesaini kiapo cha uadilifu kilichosimamiwa na kamishna wa maadili ya viongozi wa umma Salome Kaganda, huku makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan  akiwatahadharisha juu ya kusimamia vyema matumizi ya fedha za maendeleo.
Rais Magufuli pia  amewaapisha kamishna mkuu wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA,  Alphayo Kidata na Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa-Takukuru,  Valentine  Mlowola aliyewathibitisha kazini hivi karibuni baada ya kukaimu kwa muda nafasi hizo.

http://www.voaswahili.com/content/tanzania-mishahara-hewa-magufuli/3238329.html

Sunday, March 13, 2016

Arsenal yavuliwa ubingwa -FA CUP

St George na TP Mazembe nguvu sawa

Wachezaji wa TP Mazembe
Michuano ya kombe la klabu bingwa Afrika imeendelea jana kwa michezo kadhaa.
Miongoni mwa matokeo ya mechi hizo Enyimba ya Nigeria imeibugiza Vitaloo ya Burundi mabao 5-1, St George ya Ethiopia imetoshana nguvu na TP Mazembe ya Drc Congo bao 2-2, Union Douala ya cameroon imechapwa bao 1-0 na Zamalek ya Misri.
Na katika Michuano ya kombe la shirikisho Klabu ya St Eloi Lupopo ya D R Congo imeifunga Ahli Shendi ya sudani bao 2-1, Al Ittihad ya Libya imeichabanga Medeama ya Ghana bao 1-0, na Nasarawa ya Nigeria imeichapa Costantine ya Algeria bao 1-0.
Michuano hiyo inatarajia kuendelea tena march 18 mwaka huu.

Arsenal yavuliwa ubingwa -FA CUP

Michuano ya FA Iliendelea tena jana kwa mabingwa wake Arsenal kuvuliwa ubingwa baada ya kuchapwa na Watford kwa mabao 2-1.




Mabao ya Watford yalifungwa na Odion Ighalo na Adlene Guedioura huku bao la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Danny Welbeck.
Katika mchezo mwingine Manchester United wakiwa nyumbani walibanwa mbavu na West Ham united kufuatia sare ya bao 1-1.


Goli la West Ham lilifungwa na mchezaji Dimitri Payet dakika ya 68 kipindi cha pili, huku bao la kusawazisha la Manchester United likipachikwa na Anthon Martial Dakika ya 83 kipindi cha pili.

Nyumba za chama cha CCM zachomwa Pemba, Zanzibar

Watu wasiojulikana wamechoma moto nyumba za Chama Cha Mapinduzi kisiwani Pemba huku duru ya pili ya uchaguzi ikitarajiwa Machi 20.
Kamishena wa polisi wa eneo la Pemba Kusini Mohamed Shakani amesema watu hao wamechoma maeneo 11 ya kufanyia mikutano na zahanati moja lakini hakuna aliyejeruhiwa.
Amesema mshukiwa mmoja kwa jina Mohamed Ramadhan Seif amekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Shakani anasema uchunguzi wa mwanzo umeonyesha kuwa waliotekeleza kitendo hicho walinyunyiza petroli kwenye nyumba hizo katika barabara ya Kibirizi pamoja na maeneo ya mikutano ya Kiwani na Mwambe na kuwasha moto.
Waziri kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais Mohamed Aboud Mohamed amezuru maeneo hayo na kuwataka raia kusaidia kuwatambua waliotekeleza uchomaji huo.

http://swahili.cri.cn/141/2016/03/13/1s151664.htm 

Tanzania yajinasibu kuhusu takwimu kwenye ajenda 2030

Dokta Albina Chuwa, Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi
 ya Taifa ya Takwimu Tanzania. Picha: Kiswahili Unit
Mkutano wa 47 wa kamisheni ya takwimu ya Umoja wa Mataifa ukifikia ukingoni leo, Tanzania imesema imeshaandaa mpango wa ufuatiliaji wa masuala ya takwimu kwenye utekelezaji wa ajenda 2030 iliyopitishwa mwaka jana.
Akihojiwa na Idhaa hii kando ya mkutano huo uliopitisha viashiria vya kitakwimu vya kufuatilia malengo 17 ya ajenda hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ofisi ya Taifa ya takwimu nchini Tanzania Dkt. Albina Chuwa amesema mara baada ya kupitishwa kwa ajenda hiyo, waliitisha kikao cha wadau wanaozalisha na kutumia takwimu ili kuelezea mwelekeo unaotakiwa na sasa..
Na kuhusu takwimu na mabadiliko ya tabianchi kwa mujibu wa ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa iliyowasilishwa kwenye mkutano huo Dokta


http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/2016/03/tanzania-yajinasibu-kuhusu-takwimu-kwenye-ajenda-2030/#.VuWuIlKbkdU

TFF YAMALIZA MKUTANO WAKE MKUU SALAMA JIJINI TANGA

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) jana limefanya Mkutano Mkuu wa Mwaka katika Ukumbi wa Hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga ambapo mgeni Rasmi alikua ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza.



Katika hotuba yake kwa wajumbe wa mkutano huo, Mahiza aliushukuru uongozi wa TFF nchini kwa kuweza kuandaa mkutano mkuu mzuri na wa kisasa ambao pia ulifanyikia katika mkoa wake wa Tanga.
Akiongea na Wajumbe wa Mkutano Mkuu, Mahiza alisema TFF ina changamoto ambazo inapaswa kuzifanyia kazi na hasa katika kuendeleza soka la wanawake nchini ambalo mwamko wake bado uko chini.
Mahiza alisema, Mpira wa miguu kwa sasa ni ajira nzuri ambayo inasaidia kujikwamua kiuchumi kwa wachezaji pamoja na familia zao, na kuyaomba makampuni yajitokeze kuwekeza katika mpira wa miguu na hasa katika soka la wanawake.
“Mahitaji ya wanawake katika kushiriki/kucheza mpira wa miguu ni makubwa zaidi, tofauti na wanaume hivyo kuangalia jinsi gani wadhamini wanapatikana ili kuweza kuwasaidia wanawake” alisema Mahiza.
Mkutano ulijadili Ajenda za kawaida ambazo ni Kufungua Mkutano ni Uhakiki wa Wajumbe, Kuthibitisha Muhtsari wa Mkutano Mkuu uliopita, Yatokanayo na Mkutano uliopita, Hotuba ya Rais, Taarifa kutoka kwa Wanachama, Kuthibitisha ripoti ya utekelezaji wa Kamati ya Utendaji.

Zingine ni Kuthibitisha ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu 2013, Kuthibitisha ripoti ya Kamati ya Ukaguzi wa Hesabu, Kupitisha bajeti ya 2015, Marekebisho ya Katiba, Mengineyo na Kufunga Mkutano.
Baada ya majadiliano ya kina mkutano mkuu pia uliazimia kuahirisha ajenda ya marekebisho ya Katiba hadi Mkutano Mkuu ujao utakaofanyika mwezi Disemba mwaka huuu.


Wakati huo huo Leo Jumapili asubuhi Mkuu wa Mkoa Tanga, Mwantumu Mahiza ameweka jiwe la msingi katika eneo la kituo cha michezo cha kukuzia vipaji lilipo eneo la Mikanjuni jijini Tanga.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa uwekaji jiwe la msingi, Mahiza alisema wamejisikia faraja mkoa wa Tanga kupata nafasi hiyo kuwa mkoa wa kwanza kupata kituo cha kukuzia vipaji nchini.
Mahiza alisema uongozi wa Serikali mkoa wa Tanga utashirikiana na Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tanga (TRFA)/TFF katika kusaidia usimamizi wa uendeshaji wa kituo hicho.
Mahiza ameishukuru TFF kwa kuamua kuwekeza katika ujezi wa kituo hicho, ambacho baaade kitatoa nafasi kwa vijana kupata ajira kupitia mpira na shughuli nyingine za maendeleo ya kiuchumi ikiwemo utalii na watu kupata ajira katika kituo hicho.

http://tff.or.tz/news/372-tff-yamaliza-mkutano-wake-mkuu-salama-jijini-tanga

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
  2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
  4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
  5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
  6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
  7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
  8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
  9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
  10. 10.  Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
  11. 11.  Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
  12. 12.  Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
  13. 13.  Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).

Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016

http://www.ikulu.go.tz/index.php/media/news_details/2399
Picha   http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2016/02/19/160219170013_john_magufuli_tanzania_640x360_statehousetanzania.jpg