VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Sunday, April 17, 2016

Filamu nyingine ya Avatar kuongezwa

Watengenezaji wa filamu ya Avatar franchise wamesema kutatolewa filamu zaidi katika mwendelezo huo wa filamu, filamu ijayo ikitarajiwa kutolewa 2018.
Mwelekezi wa filamu hizo James Cameron ametangaza kwamba filamu hizo zitaendelezwa hadi makala ya tano itakayotolewa 2023.
Alikuwa tayari amethibitisha kwamba filamu tatu zaidi zingetolewa lakini amefichua kwamba kuna mambo mengi sana ya kuelezwa kwenye hadithi hiyo na makala zijazo tatu hazitoshi.
Kote duniani, Avatar inasalia kuwa filamu iliyofanikiwa zaidi katika historia.
Filamu hiyo imezoa $2.7bn tangu kutolewa wake 2009.
Filamu ijayo ya Avatar itatoka 2018, na hizo nyingine 2020, 2022 na 2023.

http://www.bbc.com/swahili/habari/2016/04/160416_avatar_fifth

0 comments:

Post a Comment