VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Sunday, March 13, 2016

Arsenal yavuliwa ubingwa -FA CUP

St George na TP Mazembe nguvu sawa

Wachezaji wa TP Mazembe
Michuano ya kombe la klabu bingwa Afrika imeendelea jana kwa michezo kadhaa.
Miongoni mwa matokeo ya mechi hizo Enyimba ya Nigeria imeibugiza Vitaloo ya Burundi mabao 5-1, St George ya Ethiopia imetoshana nguvu na TP Mazembe ya Drc Congo bao 2-2, Union Douala ya cameroon imechapwa bao 1-0 na Zamalek ya Misri.
Na katika Michuano ya kombe la shirikisho Klabu ya St Eloi Lupopo ya D R Congo imeifunga Ahli Shendi ya sudani bao 2-1, Al Ittihad ya Libya imeichabanga Medeama ya Ghana bao 1-0, na Nasarawa ya Nigeria imeichapa Costantine ya Algeria bao 1-0.
Michuano hiyo inatarajia kuendelea tena march 18 mwaka huu.

Arsenal yavuliwa ubingwa -FA CUP

Michuano ya FA Iliendelea tena jana kwa mabingwa wake Arsenal kuvuliwa ubingwa baada ya kuchapwa na Watford kwa mabao 2-1.




Mabao ya Watford yalifungwa na Odion Ighalo na Adlene Guedioura huku bao la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Danny Welbeck.
Katika mchezo mwingine Manchester United wakiwa nyumbani walibanwa mbavu na West Ham united kufuatia sare ya bao 1-1.


Goli la West Ham lilifungwa na mchezaji Dimitri Payet dakika ya 68 kipindi cha pili, huku bao la kusawazisha la Manchester United likipachikwa na Anthon Martial Dakika ya 83 kipindi cha pili.

0 comments:

Post a Comment