VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Friday, March 11, 2016

Rais MAGUFULI aagiza BOT kusitisha malipo ya Bil 925.9



Rais Dkt. JOHN MAGUFULI ameiagiza Benki kuu ya Tanzania BOT, kusitisha malipo ya shilingi Bilioni 925.6 ambayo tayari yalishaidhinishwa na badala yake yarejeshwe Wizara ya fedha na Mipango kwa ajili ya kufanyiwa uhakiki.
Rais Dokta MAGUFULI ametoa agizo hilo, katika ziara yake ya kushtukiza katika BOT, na kuzungumza na watendaji wakuu wa Benki hiyo waliojumuisha Gavana, Naibu Magavana, Wakurugenzi na Mameneja.Wakati huo huo, Rais Dkt. JOHN MAGUFULI amemuagiza Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. BENO NDULU, kupitia upya orodha ya wafanyakazi wa Benki hiyo, na kuwaondoa mara moja wale wote ambao hawana ulazima wa kuwa wafanyakazi katika benki hiyo.

Chanzo: https://web.facebook.com/tbconetanzania/?fref=nf

0 comments:

Post a Comment