VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Friday, March 11, 2016

Juhudi Za Kurejesha Takribani Wafungwa elfu Tatu Nchini Zaendelea

Wakenya wanaotumikia vifungo gerezani katika mataifa ya kigeni wanatarajiwa kurejeshwa hapa nchini kukamilisha vifungo vyao iwapo kutakuwa na maafikiano kati ya Kenya na nchi ambao wakenya wamefungwa gerezani. Hii ni baada ya kuratibiwa kwa rasimu ya mkataba wa maelewano kuhusu kuhamishwa kwa wafungwa wa Kenya. Rasimu hiyo ya mkataba inaratibiwa na afisi ya mkuu wa sheria chini ya uongozi wa mwanasheria mkuu, Prof Githu Muigai. Stakabadhi hiyo itabuni msingi wa utekelezaji wa sheria ya kuwahamisha wafungwa ya mwaka 2015 iliyoanza kutekelezwa tarehe-12 mwezi Oktoba mwaka 2015. Pindi mikakati ya kisheria itakapobuniwa, Wakenya wanaotumikia vifungo katika mataifa ya kigeni watarejeshwa hapa nchini kukamilisha vifungo hivyo. Mkataba huo pia unatarajiwa kuratibisha matakwa ya kubadilishana wafungwa. Inakadiriwa kuwa wakenya elfu-3 wanatumikia vifungo katika mataifa ya kigeni huku magereza ya humu nchini pia yakiwa na idadi sawia ya wafungwa wa kigeni.












Juhudi Za Kurejesha Takribani Wafungwa elfu Tatu Nchini Zaendelea 
Chanzo:http://radiotaifa.co.ke/index.php/juhudi-za-kurejesha-takribani-wafungwa-elfu-tatu-nchini-zaendelea/

0 comments:

Post a Comment