VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Thursday, March 10, 2016

Dokta JOHN MAGUFULI amesisitiza umuhimu wa TANZANIA kujifunza mbinu mbalimbali kutoka VIETNAM

Tanzania na Vietnam zakubaliana kushirikiana katika sekta mbalimbali
TANZANIA na VIETNAM zimekubaliana kushirikiana katika nyanja za mawasiliano, elimu, kilimo, biashara na uvuvi ili kukuza uchumi wa nchi zote mbili ambazo zina mahusiano kwa takribani Miaka HAMSINI sasa.
Hayo yamebainishwa na viongozi wa nchi hizo Rais JOHN MAGUFULI pamoja na Rais TROUNG TANG SAN wa VIETNAM wakati wa dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa kwa ajili ya Rais huyo wa VIETNAM Ikulu Jijini DSM.
Akizungumza katika dhifa hiyo Dokta JOHN MAGUFULI amesisitiza umuhimu wa TANZANIA kujifunza mbinu mbalimbali kutoka VIETNAM ambazo nchi hiyo ilizitumia na kuweza kukuza uchumi wake.
Kwa upande wake Rais TRUONG TANG SAN ambaye anafanya ziara ya kwanza Barani Afrika huku akiwa rais wa pili wa nchi hiyo kuzuru TANZANIA tangu mwazoni mwa Miaka ya SABINI amesisitiza kuwa uhusiano uliojengwa na waasisi wa mataifa haya mawili lazima uenziwe na kulindwa kwa manufaa ya wananchi wa nchi zote mbili..


https://web.facebook.com/tbconetanzania/


0 comments:

Post a Comment